Siku ya jana shirikisho la soka ulimwenguni FIFA liliweza kutangaza washindi wa tuzo kubwa ikiwa ni pamoja na tuzo ya mchezaji bora wa Dunia ambayo ilikuwa na ushindani mkubwa ikiwa inawaniwa na Lionel Messi, Neymar na Cristiano Ronaldo.
Usiku wa jana FIFA wali mtangaza mshambuliaji wa kimataifa wa Argentina na mchezaji wa klabu ya FC Barcelona kutoka Hispania Lionel Messi kuwa ndio mshindi wa tuzo ya mchezaji bora wa Dunia ikiwa ni mara ya tano kwake kuchukua Tuzo hiyo.
HII HAPA OODHA YA WASHINDI WENGINE WA TUZO ZA FIFA 2015
- Golikipa: Manuel Neuer,
Mabeki: Thiago Silva, Marcelo, Sergio Ramos, Dani Alves
Viungo: Andres Iniesta, Luka Modric, Paul Pogba,
Washambuliaji: Neymar, Lionel Messi, Cristiano Ronaldo. - KIKOSI BORA CHA MWAKA.

- Tuzo ya Kocha bora wa mwaka ilchukuliwa na Luis Enrique wa FC Barcelona.
- Tuzo bora ya goli la mwaka alichukua Wendell Lira wa klabu ya Atletico Goianiense
- Tuzo ya Mchezaji bora wa mwaka wa kike alichukua Carli Lloyd kwa mara ya kwanza kutoka USA.
LIONELL MESSI MSHINDI WA BALLON D'OR MARA YA TANO
Reviewed by Unknown
on
02:22
Rating:

No comments: